Ruka uende katika maudhui ya msingi

Last modified: 13/10/2025

Mwongozo wa Uber wa Mamlaka ya Utekelezaji Sheria - Nje ya Marekani

Uber imeahidi kuendelea kuboresha usalama wa mfumo wetu na kuchangia usalama katika jumuiya ambazo tunazitolea huduma. Uber ina timu mahususi inayofanya kazi na mashirika ya utekelezaji sheria kote ulimwenguni, Timu ya Mwitikio wa Usalama wa Umma (“PSRT”). Timu hii hukagua na kujibu kila ombi la utekelezaji sheria linalopokelewa na Uber. Timu ya PSRT ina michakato ya kusaidia utekelezaji sheria wakati wowote kila siku, ikiwa ni pamoja na maombi ya dharura, kupitia Tovuti yetu ya Usalama wa Umma, au kupitia barua pepe kwa LERT@uber.com.

Uber pia imeahidi kuzingatia faragha ya data ya watumiaji wetu. Uber huhifadhi na kudumisha data ya mtumiaji kama ilivyoelezwa kwenye Ilani yetu ya Faragha na Sheria na Masharti yanayohusika katika kila eneo la mamlaka ambapo Uber inatoa huduma. Uber hufichua data kwa watekelezaji sheria kwa mujibu wa sheria husika na kanuni za msingi za Uber.

Maelezo ya hivi karibuni kuhusu bidhaa na huduma za Uber yanapatikana katika Kituo chetu cha Msaada na Chumba cha Habari.

Mwongozo huu na Maswali Yanayoulizwa Sana yanayoambatana, hayakusudiwi kutoa ushauri wa kisheria. Pia haijumuishi haki zozote zinazoweza kutekelezwa na Uber ina haki ya kusasisha au kubadilisha mwongozo huu bila ilani kwa watekelezaji sheria.

Muhtasari wa PSRT

Uber Technologies, Inc. (“UTI”) na Uber BV ni wadhibiti wa pamoja wa data yote ya binafsi ya mtumiaji katika Nchi Zanachama za Muungano wa Ulaya (“EEA”), Uswisi na Uingereza, na UTI ndiyo mdhibiti pekee wa data kwa data nyingine zote. Timu ya Uber ya PSRT huchakata maombi kutoka kwa watekelezaji sheria kote ulimwenguni, kwa mujibu wa maelekezo ya mdhibiti wa data husika.

Baada ya kupokea mchakato wa kisheria, ombi la kuhifadhi, au ombi la ufichuaji wa dharura, Uber inaweza kufichua data iliyoombwa ikiwa kufanya hivyo kutalingana na:

  • sheria ya Marekani, ikiwa ni pamoja na Sheria ya Faragha ya Mawasiliano ya Kielektroniki;
  • sheria ya nchini ya mamlaka yanayotuma ombi na sheria nyingine zozote zinazohusika, kama vile Kanuni ya Jumla ya Ulinzi wa Data ya Umoja wa Ulaya (GDPR);
  • Kanuni za msingi za Uber, kama ilivyoelezwa hapa chini; na
  • Sera za watumiaji wa Uber, ikiwa ni pamoja na Ilani ya Faragha na Sheria na Masharti yanayohusika.

Watekelezaji sheria wanapaswa kutumia Tovuti kama njia ya msingi ya kuwasiliana na PSRT. Tovuti hii hutoa njia kuu ya mawasiliano kwa watekelezaji sheria kuwasiliana na wataalamu wa PSRT wakati wa kuwasilisha mchakato wa kisheria, maombi ya kuhifadhi au maombi ya ufichuaji wa dharura. Watekelezaji sheria pia wanaweza kutumia Tovuti kupata maelezo ya hali kuhusu mchakato wa kisheria uliowasilishwa au kuuliza maswali. Maelekezo ya kufungua akaunti yanapatikana hapa. Watekelezaji sheria na wafanyakazi wa serikali walioidhinishwa kupata ushahidi unaohusiana na mashtaka rasmi ya kisheria ndio tu wanaoweza kutumia Tovuti. Akaunti za tovuti zinapaswa kufunguliwa kwa kutumia watekelezaji sheria rasmi au akaunti ya barua pepe ya serikali. Pia unaweza kuwasiliana na PSRT kupitia LERT@uber.com. Maombi ya barua pepe lazima yawasilishwe kutoka kwa watekelezaji sheria rasmi au akaunti ya barua pepe ya serikali na yajumuishe jina la afisa wa utekelezaji sheria anayeomba, cheo, nambari ya beji au kitambulisho sawa na hicho (ikiwa kinahusika), wakala na maelezo ya mawasiliano ya moja kwa moja.

Mahitaji ya Mchakato wa Kisheria, Maombi ya Uhifadhi na Maombi ya Ufichuaji wa Dharura

Wakati wa kuwasilisha ombi lolote kwa Uber, watekelezaji sheria wanapaswa kubaini akaunti mahususi iliyohusishwa na ombi hilo. Inapowezekana, watekelezaji sheria wanapaswa kutoa kitambulisho cha kipekee kinachohusishwa na akaunti kama vile anwani ya barua pepe, namba ya simu na/au namba pleti ya gari. Majina pekee mara nyingi huwa si vitambulishi vya kipekee, wala tarehe za kuzaliwa (kwa kiwango kilichokusanywa). Uber pia inaweza kubaini akaunti zinazohusika na uchunguzi wa utekelezaji sheria kwa kutafuta maelezo yanayohusiana na safari mahususi. Kwa maombi kama hayo, maelezo kuhusu safari hiyo, kama vile maelezo ya kumtambulisha mtumiaji aliyetajwa hapo juu na tarehe, wakati, kitambulisho cha safari au mahali pa kuchukuliwa au kushushwa.

Mchakato wa kisheria, maombi ya kuhifadhi na maombi ya ufichuaji wa dharura lazima yatumwe kwenye taasisi ya Uber inayofaa:

  • Maombi kutoka kwa mamlaka ya EEA, Uswisi na Uingereza yanapaswa kutumwa kwa Uber B.V., Burgerweeshuispad 301, 1076 HR, Amsterdam, Uholanzi.
  • Maombi kutoka kwa mamlaka mengine yote yanapaswa kutumwa kwa Timu ya Usalama wa Umma, Uber Technologies, Inc. (UTI), 1725 3rd Street, San Francisco, CA 94158.

Mchakato wa Kisheria

Maombi yote ya utekelezaji sheria ya data lazima yathibitishwe na mchakato wa kisheria (isipokuwa maombi ya dharura, yaliyojadiliwa hapa chini). Uber ina haki ya kukataa mchakato wa kisheria kwa sababu yoyote, ikiwa ni pamoja na maombi ambayo hayana msingi halali wa kisheria, yenye maelezo mengi, hayaeleweki, au hayafai kwa namna nyingine, au ikiwa Uber haiwezi kuthibitisha uhalali wa ombi. Uber pia inaweza kuhitaji amri halali ya mahakama ya Marekani (kupitia mkataba wa msaada wa kisheria wa pamoja, makubaliano ya msaada wa kisheria wa pamoja au ombi rasmi la mahakama) kufichua aina fulani za rekodi kwa mamlaka yaliyo nje ya Marekani. Kwa mfano, Uber kwa ujumla huhitaji amri halali ya mahakama ya Marekani (kupitia mkataba wa msaada wa kisheria wa pamoja, makubaliano ya usaidizi wa kisheria wa pamoja au barua rasmi kutoka mahakamani) ili kufichua maudhui ya mawasiliano kwa mamlaka yaliyo nje ya Marekani.

Ili kuwa halali, mchakato wa kisheria uliowasilishwa kwa Uber lazima kwa jumla:

  • utumwe kwa asasi ya Uber inayofaa;
  • utolewe kwa kutii sheria ya eneo husika la mamlaka yanayoomba;
  • utolewa na mamlaka yanayofaa, kama vile jaji;
  • utiwe saini na mamlaka yanayofaa, kama vile jaji;
  • uwe na tarehe;
  • utoe tarehe ya kurudisha hati za kuwasilisha, ikiwa inahitajika; na
  • ubainishe akaunti inayolengwa, iliyotambuliwa kwa njia inayofaa; aina ya maelezo kwenye akaunti itakayofichuliwa; na tarehe yoyote inayohusika.

Maombi ya Kuhifadhi

Utekelezaji wa sheria unaweza kuomba uhifadhi wa rekodi za akaunti. Baada ya kupokea ombi kama hilo, Uber inaweza kuchukua hatua za kuhifadhi rekodi zozote au maelezo mengine iliyo nayo kuhusu tatizo la ombi la kuhifadhi, wakati mchakato wa kisheria unasubiri. Hifadhi ni “picha” ya mara moja ya rekodi au maudhui katika akaunti ya mtumiaji wa Uber wakati tunapokea ombi la kuhifadhi; si hifadhi inayoendelea ya wakati halisi wa rekodi hizo. Uber ina haki ya kukataa maombi ya uhifadhi kwa sababu yoyote.

Maombi ya Ufichuaji wa Dharura

Kwa kiwango kinachopatana na sheria za Marekani na mitaa, Uber inaweza kufichua data ya mtumiaji kwa hiari kwa chombo cha utekelezaji wa sheria ikiwa Uber ina imani ya nia njema kwamba dharura inayojumuisha hatari ya kifo au majeraha makubwa ya kimwili kwa mtu yeyote inahitaji ufichuaji bila kuchelewesha maelezo yanayohusiana na dharura. Lazima data iliyoombwa iwe tu data inayohitajika kushughulikia haswa dharura inayoendelea.

Maombi ya ufichuji wa dharura yanaweza kuwasilishwa kupitia Tovuti, au kupitia barua pepe pamoja na Fomu ya Ufichuaji wa Dharura iliyoambatishwa. Kwa sababu ya ahadi yake ya kudumisha usalama kwenye mfumo wake, Uber ina michakato ya kujibu maombi ya dharura wakati wowote kila siku.

Ili kuwasilisha ombi la kufichua maelezo ya dharura, lazima watekelezaji wa sheria:

  • wathibitishe kwamba wameidhinishwa na sheria kuchukua rekodi zilizoombwa;
  • wathibitishe kwamba ombi hilo linahusiana na hali ya dharura inayohusisha hatari ya kifo au jeraha kubwa la kimwili ambalo linahitaji ufichuaji bila kuchelewesha maelezo yanayohusiana na dharura hiyo;
  • waseme kwamba kuna hatari kubwa ya dharura kuweza kutokea ikiwa kuna ucheleweshaji unaosababishwa na kupata mchakato halali wa kisheria wa mahali ulipo;
  • wabainishe akaunti inayolengwa, iliyotambuliwa kwa njia inayofaa; aina ya maelezo kwenye akaunti yatakayofichuliwa; na tarehe yoyote inayohusika; na
  • ikiwa inahitajika kwa mujibu wa sheria, wafuate mchakato wa kisheria.

Uber hutathmini maombi ya ufichuaji wa dharura kulingana na hali, ikiwa ni pamoja na hali ya dharura na itaamua kwa hiari yake pekee ikiwa itatoa data inayotafutwa. Uber inaweza kuomba maelezo ya ziada au hati ili kusaidia katika tathmini ya ombi la ufichuaji wa dharura.

Sera ya Ilani ya Mtumiaji ya Uber

Uber inaweza kuwaarifu watumiaji kuhusu maombi ya utekelezaji sheria kwa data yao, isipokuwa ikiwa ilani hairuhusiwi kwa mujibu wa sheria inayohusika.

Kama sehemu ya taratibu za uchunguzi wa usalama wa Uber, Uber inaweza kuchagua kuwasiliana na mtu aliyetambuliwa katika ombi la utekelezaji sheria kuhusiana na tukio lolote linalodaiwa kuwa la usalama. Uber haitaanzisha mawasiliano kama hayo ikiwa inaamini, kwa busara yake pekee, kwamba mawasiliano kama hayo yanaweza:

  • kuwa hatari ya majeraha makubwa au kifo kwa mwananchi; au
  • kupotosha njia ya haki au kuathiri utoaji wa haki.

Wakati wa kuwasilisha ombi, watekelezaji sheria wanaweza kuomba Uber isiwasiliane na mtu yeyote anayehusishwa na ombi kutokana na sababu zilizotajwa au sababu nyingine halali kulingana na kesi itakavyokuwa.

Kanuni za Msingi za Uber

Uber hutathmini maombi kutoka kwenye mamlaka ya utekelezaji sheria nje ya Marekani kwa kurejelea kanuni za msingi za Uber. Uber huenda isifichue data ikiwa kufanya hivyo hakupatani na kanuni hizo.

Kanuni za msingi za Uber kwa maombi ya utekelezaji wa sheria ni pamoja na:

  1. Lazima maombi yote yazingatie sheria husika na yawekwe ipasavyo.
  2. Uber haitawezesha ufikiaji wa wakati halisi na unaoendelea wa data sahihi na isiyobadilika ya safari kwa kuruhusu ufikiaji usiosimamiwa wa mifumo yake ya ndani.
  3. Maombi yanayohusiana na uchunguzi wa uhalifu lazima yahusishe tabia ambayo inaweza kusababisha uhalifu nchini Marekani na nchi anayoishi mhusika, isipokuwa kwa maombi yanayohusiana na ufichuaji wa data ya mtumiaji wa EEA, Uswisi na Uingereza. Katika mamlaka haya, uchunguzi wa uhalifu lazima uhusishe tabia ambayo inaweza kusababisha uhalifu nchini Uholanzi au Marekani, pamoja na nchi anayoishi mlengwa.
  4. Sheria za mitaa lazima zitoe utaratibu wa kupinga mchakato wa kisheria.

Maelezo Yanayopatikana Kutoka Uber

Sehemu hii inaelezea aina za jumla za data ya mtumiaji zinazoweza kupatikana kutoka Uber. Inakusudiwa kutoa mwongozo kuhusu baadhi ya aina za data zinazoombwa kwa kawaida, na haukusudiwi kuwa kamili. Kwa maelezo ya ziada kuhusu bidhaa za Uber, tafadhali angalia ukurasa wa Bidhaa ya Uber.

Uber hukusanya na kudumisha data ya mtumiaji kwa mujibu wa Ilani ya Faragha na Sheria na Masharti yanayohusika. Data inayokusanywa na kuhifadhiwa na Uber inaweza kutofautiana kutoka akaunti moja hadi nyingine, kama vile mtumiaji wa Uber anapofuta maelezo ya akaunti yake. Kwa hivyo, aina za data ambazo Uber hutoa wakati wa kukabiliana na mchakato halali wa kisheria zinaweza kutofautiana.

Maelezo ya Msingi ya Msajiliwa

Maelezo ya msingi ya mteja yanayohifadhiwa na Uber kwa ajili ya wasafiri na madereva yanaweza kujumuisha:

  • jina;
  • anwani ya barua pepe;
  • namba ya simu;
  • tarehe ya kufungua akaunti; na
  • hali ya akaunti.

Maelezo ya Kifaa

Maelezo ya kifaa yanajumuisha maelezo kuhusu kifaa cha mkononi cha mtumiaji.

Maelezo ya Gari

Maelezo ya gari ambayo Uber inaweza kutoa ni pamoja na:

  • data ya namba pleti ya gari;
  • aina na muundo;
  • bima ya gari;
  • usajili wa gari; na
  • mamba ya utambulisho wa gari (VIN).

Maelezo ya Malipo

Njia na chanzo cha maelezo ya malipo ambayo Uber inaweza kutoa ni pamoja na:

  • kadi ya mikopo (nambari sita za kwanza na nne za mwisho za kadi ya mikopo) au nambari za akaunti ya benki (madereva na wasafirishaji bidhaa pekee);
  • tarehe ya mwisho ya kutumia kadi ya mikopo;
  • msimbo husika wa eneo wa kadi ya mikopo; na
  • njia nyingine za malipo.

Maelezo mengine ya malipo ambayo Uber inaweza kutoa ni pamoja na:

  • maelezo kuhusu miamala mahususi, kama vile kiasi, tarehe na wakati ambapo muamala ulifanyika na njia ya malipo iliyotumika.

Maelezo ya Safari

Maelezo ya safari kwa ujumla ni pamoja na:

  • mchanganuo wa kiasi kinachotozwa msafiri kwa ajili ya safari;
  • maeneo ya kuchukuliwa na kushushwa (latitudo na longitudo); na
  • maelezo kuhusu msafiri na dereva, ikiwa ni pamoja na jina na ukadiriaji. Kumbuka kwamba madereva na wasafiri huweka majina yao kama inavyoonekana katika programu, kwa hivyo si lazima yawe majina yao au yanaweza kufupishwa (kwa mfano “Chris” la “Christopher”).

Maelezo ya Mahali

Uber inaweza kukusanya maelezo ya mahali ya GPS kutoka kwenye vifaa vya mkononi vya madereva na wasafiri wake. Maelezo ya mahali ya dereva yanaweza kurekodiwa wakati programu ya Uber inafanya kazi kwenye simu ya dereva wakati safari ni ye mtandaoni au nje ya mtandao, mradi tu dereva ameingia katika akaunti kwa ajili ya kupokea safari. Katika mipangilio ya vifaa vyao, wasafiri wana chaguo la kujiondoa kwenye ukusanyaji wa maelezo yao ya GPS na wakichagua kufanya hivyo, GPS ya msafiri haitarekodiwa.

Maelezo ya Wasifu wa Mtumiaji

Maelezo mengine ya wasifu wa mtumiaji kuhusu mtumiaji ambayo Uber inaweza kutoa ni pamoja na:

  • ukadiriaji (nyota moja hadi tano);
  • majibu/maoni yaliyoandikwa; na
  • picha za wasifu.

Maelezo ya Wasifu wa Dereva

Uber inaweza kuhifadhi maelezo yafuatayo kuhusu dereva wake:

  • tarehe ya kuzaliwa;
  • maelezo ya gari (kama ilivyoelezwa hapo juu); na
  • namba ya leseni ya dereva

Maelezo ya Mawasiliano

Uber inaweza kunasa maelezo fulani kuhusu mawasiliano kati ya watumiaji wake kwenye programu ya Uber, kama vile wakati dereva na msafiri wanatumia programu kuwasiliana wao kwa wao. Hii inaweza kujumuisha rekodi zisizo za maudhui zinazohusishwa na mawasiliano kama hayo, au katika hali ya ujumbe wa maandishi kupitia programu, maudhui ya mawasiliano hayo.

Rekodi za mawasiliano zinaweza kuwa ni pamoja na:

  • maelezo ya kwa/kutoka; na
  • tarehe na wakati wa mawasiliano.

Maudhui ya mawasiliano yanaweza kujumuisha ujumbe unaotumwa kati ya watumiaji kwenye programu.

Rekodi za Huduma kwa Wateja

Rekodi za huduma kwa wateja ambazo Uber inaweza kuhifadhi ni pamoja na:

  • rekodi za simu za usaidizi kwa wateja; na
  • mawasiliano mengine ya usaidizi kwa wateja.

Rekodi Nyingine za Biashara

Rekodi nyingine za biashara ambazo Uber inaweza kuhifadhi ni pamoja na:

  • nakala za leseni ya dereva.

Maelezo Yanayohusishwa na Huduma Nyingine za Uber

Uber inaweza kutoa aina nyingine za maelezo kuhusu watumiaji wa huduma zake nyingine.

Uber Eats:

  • maelezo ya msingi ya mteja;
  • maelezo ya mgahawa;
  • maelezo ya mawasiliano ya mgahawa au mmiliki;
  • historia ya kuagiza; na
  • maudhui ya mawasiliano kati ya watumiaji na wasafirishaji wa Uber Eats.

Uber Freight:

  • kumbukumbu za simu kati ya Uber na msafirishaji;
  • maandishi kati ya Uber na msafirishaji;
  • maelezo ya mawasiliano ya Uber;
  • kupakia maelezo (kwa mfano, asili, mahali unakoenda, bidhaa zilizo kwenye shehena); na
  • Maelezo ya eneo la GPS (tofauti na usafiri wa pamoja, madereva hawahitajiki kuingia kwenye akaunti wakati wa kusafirisha bidhaa; kwa hivyo, data ya GPS inaweza kupatikana au isipatikane).

Uber inaweza kukupa data ya ziada ambayo haijaorodheshwa hapa. Maombi ya utekelezaji sheria yanapaswa kuwa na maelezo bayana kuhusu data inayoombwa, kulingana na mwongozo uliotolewa hapo juu.

Maswali Yanayoulizwa Sana (FAQ)

Swali: Ninaweza kuwasilisha vipi mchakato wa kisheria kwa Uber?

A: Mchakato wa kisheria, maombi ya kuhifadhi na/au maombi ya ufichuaji wa dharura yanapaswa kupakiwa kupitia Tovuti ya Usalama wa Umma ya Uber. Tovuti husaidia kuthibitisha kwamba mwombaji ameidhinishwa kutuma ombi, kwa kuwa anatumia idara, wakala au anwani ya barua pepe ya serikali yake kusajili akaunti ya Tovuti. Tovuti hii husaidia Uber kukusanya maelezo yanayohitaji ili kuchakata maombi ya utekelezaji wa sheria kwa haraka na inatoa vipengele muhimu kwa watekelezaji sheria, kama vile uwezo wa kufuatilia hali ya maombi yao au kuwasiliana na PSRT. Maombi pia yanaweza kuwasilishwa kupitia barua pepe, kwa LERT@uber.com.

Swali: Je, unawaarifu watumiaji kuhusu mchakato wa kisheria?

A: Tunaweza. Kwa maelezo kuhusu sera ya ilani ya watumiaji wa Uber, angalia kifungu kidogo cha ‘Sera ya Ilani ya Mtumiaji ya Uber’ katika mwongozo ulio hapo juu.

Swali: Watekelezaji sheria wanapaswa kufanyia nini rekodi wanazopata kutoka kwa Uber baada ya uchunguzi au kesi kukamilika?

A: Maelezo yanayopatikana kutoka kwa Uber yanapaswa kuharibiwa baada ya uchunguzi au kesi kukamilika au data haihitajiki tena, yoyote inayotangulia.

Swali: Nilituma mchakato wa kisheria, lakini Uber haijajibu. Nifanyaje?

A: Tovuti ya Uber inaruhusu watekelezaji sheria kufuatilia hali ya ombi lake na kutuma maswali ya kufuatilia. Uber hupokea maelfu ya maombi kila mwaka na hukagua maombi inayopokea baada ya kupokelewa. Uber hufanya kila juhudi kujibu maombi kwa haraka.

Swali: Sera ya Uber ya kufunga akaunti ni gani? Je, Uber hufunga akaunti baada ya ombi? Je, Uber itafungua akaunti ikiombwa?

A: Kwa sababu ya ahadi yake ya kudumisha usalama kwenye mfumo wake, Uber inapofahamishwa kuhusu tukio, Uber inaweza kuchukua hatua ambazo ni pamoja na kumzuia mtu huyo kufikia mfumo. Tafadhali angalia Mwongozo wa Jumuiya ya Uber kuhusu sera za Uber za kufunga akaunti.

Swali: Je, Uber inaomba fidia kwa gharama zinazohusiana na kujibu mchakato wa kisheria?

A: Kwa sasa, kwa jumla Uber haitaki fidia ya gharama zinazohusiana na kujibu mchakato wa kisheria, ingawa ina haki ya kufanya hivyo.

Swali: Je, Uber inaweza kutoa nenosiri la akaunti ya mtumiaji?

A: Hapana, Uber haina uwezo wa kufikia manenosiri ya watumiaji.