Ruka uende katika maudhui ya msingi
11 Mei 2021

Uber imeanzisha huduma ya delivery jijini Dar

Monica Mziray
Share this article

Sasa unaweza kutumia App ya Uber kufanya delivery ya bidhaa/mizigo kwa ajili yako, rafiki zako au hata kwa ajili ya wateja wako. Ni rahisi sana kutumia huduma hii;

UberConnect ni nini?

UberConnect ni huduma ya kusafirisha mizigo/bidhaa  zako binafsi na hata za kibiashara. Sasa unaweza kufanya delivery ya vitu vyako kwa urahisi, usalama, uhakika  na kwa gharama nafuu zaidi kupitia App ya Uber.

Huduma hii itaanza rasmi tarehe 17/05/2021 na madereva wetu wa UberBODA ndio watakaokuwa wakisafirisha bidhaa hizi kwa kutumia boda boda zao, na hivyo kufanya  bei za usafirishaji kuwa sawa sawa sawa na  bei ya sasa ya huduma ya UberBODA.

Base fareTZS 700
Kwa kilometaTZS 250
Kwa dakikaTZS 55
Nauli ya chini TZS 1000

Jinsi inavyofanya kazi

  1. Fungua App ya abiria ya Uber.
  2. Chagua huduma ya Connect ndani ya app ya Uber, kubali vigezo na masharti, thibitisha kwamba mzigo wako hauna bidhaa zilizopigwa marufuku, na uite usafiri.
  3. Jibu ujumbe utakaopokea kwenye app ya Uber utakaokuomba uweke jina la mpokeaji sambamba na maelekezo mengine yoyote ambayo ungependa kumwambia dereva wako.
  4. Kutana na dereva na umkabidhi mzigo ambao unataka usafirishwe.
  5. Share safari na mtu unaetaka kumpelekea mzigo ili na yeye aweze kuifuatilia mzigo wake.

Mizigo inayosafirishwa

Ukomo wa bidhaa zinazosafarishwa kupitia Uber Connect ni kilo 15 na thamani yake isizidi TZS 115,000 na lazima zizingatie sheria na masharti yote ya serikali sambamba na sera za Uber. Ni marufuku, kutuma bidhaa haramu au bidhaa nyingine zilizopigwa marufuku.

Ukituma mzigo wowote unaokiuka sheria yoyote ya nchi au sera zetu, ikiwa ni pamoja na zile zilizoainishwa kwenye ukurasa huu, tutakuchukulia hatua za kinidhamu inavyostahili, ikiwa ni pamoja na kusitisha au kufunga akaunti yako mara moja. Unaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kama vile kushtakiwa kwa makosa ya jinai iwapo utatuma mizigo haramu au hatari.

Bidhaa zilizopigwa marufuku ni pamoja zifuatazo;

  • Bidhaa haramu.
  • Bunduki, silaha, na vipuri vya silaha.
  • Pombe, madawa ya kulevya au bidhaa za tumbaku
  • Vyakula au vinywaji vinavyoharibika haraka (kama mayai).
  • Bidhaa hatari au zenye madhara mabaya, ikiwa ni pamoja na vilipuzi, bidhaa zenye sumu au zinazowaka moto rahisi, uchafu wa hospitali na bidhaa nyingine ambazo zina madhara kama inavyoainishwa na sheria husika.
  • Pesa, kadi za zawadi (gift cards), tiketi za kamari au hisa zinazohamishika.
  • Vitu/ bidhaa za wizi.
  • Vitu ambavyo vinaweza kuvunjika kwa haraka kama glass.

    Maswali yanayoulizwa mara kwa mara;

      • UberBODA
    • Bidhaa zote halalil, zisizozidi kilo 15 na ambazo thamani yake haizidi TZS 115,000. Kikubwa zaidi bidhaa hizo zisiwe miongoni mwa zilizoorodheswa hapa

    • Dar es Salaam tu. Tutaendelea kukutumia taarifa kadri tunavyopanua wigo wetu katika maeneo mengine.

    • Ndio, unaweza kuagiza uletewe mzigo, unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha  kwamba umeweka eneo sahihi la mzigo kuchukuliwa na uweke mahali ulipo kuwa kama eneo ambako mzigo unapelekwa.

      • Ikiwa umeita usafiri, na tayari unaletewa mzigo, basi unachotakiwa kufanya ni kuufuatilia ndani ya App ya Uber.
      • Ikiwa ni mtu mwingine ndiye ameagiza mzigo kwa niaba yako, unachitakiwa kufanya ni kumwomba aliyeagiza kushare safari ili ufuatilie mzigo wako
    • Wakati una request, ukishampata dereva, slide screen yako kwenda juu utaona kuna sehemu imeandikwa “Share trip status” Bonyeza hiyo, halafu chagua namba ya mtu unaetaka kushare nae safari.

    Imeandikwa na

    Monica Mziray

    Related Articles
    0 makala
    Chuja kulingana na:
    Kategoria zote
    Hakuna makala yaliyopatikana.